Powered by Blogger.

Wednesday, 24 December 2014

MTIKISIKO MKUBWA SERIKALINII ::MAMBO MAZITO YALIOADHIMIWA NA UKAWA JUU YA JK NA KUKING'OA CHAMA TAWALAFUATILIA MKASA HUU

Posted by Unknown at 13:19 0 Comments

MH : SLAAAKIONGEA NA WAANDISHI








WAKATI wananchi wakiwa bado hawajalizika kuhusu  Hatua alizochukua Rais Jakaya Kikwete, Juu ya maamuzi ya Bunge kuhusu ufisadi wa Zaidi bilioni 306 kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow,kutokana na Rais Kikwete kulikejeri Bunge kwa kuyatupia mbali mapendekezo mengi ya Bunge .
       Nao Umoja wa Vyama vya vikuu vya Upinzani nchini ambavyo vinaunda Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi UKAWA vimeibuka na kumvaa Rais Jakaya Kikwete na kusema anahusika kwa kiasi kikubwa kwenye Ufisadi huo, kwa kitendo chake cha kumtetea Mmiliki wa wa kampuni ya Independent power  limited  (IPTL), Bwana Harbnder Singh (Singasinga)
     Na Kusema Umoja huo utaanzisha Maandamano nchi nzima kupinga Ufisadi huo ambao wanadai unalindwa na Rais Kikwete kutokana na yeye kuhusika katika Wizi huo .
        Kauli hiyo ya Vyama  hivyo vikuu vya Upinzani vinavyounda UKAWA umetolewa leo  Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Umoja huo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahimu Lipumba wakati wa mkutano na waandishi wa Habari uliohitishwa Mahususi ili kuzungumzia hutuba ya Rais Kikwete kuhusu sakata hilo ambapo –
       Profesa Lipumba alisema inasikitisha kuona Rais Jakaya Kikwete ameacha kulitetea shirika la Umeme Tanesco na kuwatetea Mataperi wa IPTL ambao wameliingizia hasara la mabilioni ya Fedha shirika  hilo.
“Hutuba ya Rais kikwete imekuwa mtetezi mkubwa wa Mmiliki wa PAP,anaacha kulitetea shirika la umma la Tanesco,harafu anadanganya umma kwa kiasi kikubwa  kusema kwamba pesa za IPTL si za Umma hivi anashindwa hata kuelewa Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Serikal CAG  ambayo inaonyesha wazi kwamba wamiliki hawa wamefanya utaperi wa wazi kabisa katika umiliki wake “
   “Taarifa za mauzo ya Kampuni ya Mechmar kwenda piper link kwenda PAP ziliwasilishwa katika taasisi mbalimbali za Serikali na bwana Singh sote tunafahamu ni kughushi nyaraka ili akwepe Kodi na hili ni kosa,hivi Kikwete alioni hili?”alihoJi Profesa lipumba.
        Profesa lipumba alizidi kusema hata Maazimio yanayotokana na Taarifa ya CAG yanaonyesha wazi kuwa PAP siyo mmiliki wa harali wa  hisa za Kampuni ya Mechmar lakini Rais Kikwete hakuliona hilo.



Kwa Upande wake Katibu  mkuu wa Muungano vyama hivyo wa Vya Upinzani vinavyounda UKAWA ambaye pia naye ni Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Dokta Wilbroad Slaa amesema Umoja umepanga kuzunguka nchi nzima ikiwemo kuandaa maandamano kupinga kile wanachodai Rais Jakaya Kikwete amewalinda wezi wa Ufisadi huo.
       Dokta Slaa aliongeza kuwa Kitendo cha Rais kikwete kuwatetea Wamiliki wa kampuni ya IPTL ni wazi Rais Kikwete anahusiki kutokana na kuwepo kwa ushahidi wa yeye kuhusika na Wezi huo.
     “Tunajua wazi kwamba Rais kikwete kuhusika na wizi huu kwani kunamtu mmoja anaitwa Guruma ambaye katika watu waliopewa pesa na bwana James Rugimalira jina lake limetajwa kupokea mabilioni ya Fedha na mtu huyo mimi namfahamu sana,Bwana Guruma anajulikana sana ni msimamizi wa Miradi ya Rais kikwete na leo kachukua pesa za Escrow unategemea nini hapa na ndio maana anasuasua kuwachukulia hatua wamiliki wa IPTL”Alisema Dokta Slaa.
        Aidha,Dokta Slaa alisema kitendo cha Ufisadi huo kutokea  na Idara ya Usalama wa Taifa kushindwa kulinda  nchi kwenye ufisadi huo ni wazi idara hiyo imeshindwa kazi.
    “Usala wa Taifa upo kila Barozi inashangaza sana kuona Idara hii inashindwa kuona utaperi wa mmiliki wa IPTL au tutegemee nini ndio maana hata kwenye Ufisadi wa EPA,tuliona Jinsi Kampuni iliyokuwa ikimilikiwa na Ofisa wa Usalama wa Taifa ilivyochota pesa unategemea nini”
       “Na hata Kikwete alivyosema mara baada ya kutua uwanja wa ndege  alipotoka kutibiwa anavyosema alijui sakata hili kutokana na yeye kuwa kwenye matibabu , ni kuwadanganya watanzania kwani baada ya masaa mawili kutoa uwanja wa ndege  hapo,niliona email aliyekuwa akitumiana na bwana Rugimalira,sasa huyo ni kiongozi kweli”alihoji Dokta Slaa.
 

Naye Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi James Mbatia alisema ni Rais kikwete amekosa maamuzi katika nchi kutokana na kitendo chake cha kushindwa kuwachukulia hatua waliohusika na kusema pesa za wananchi zimepotea huku taifa likiosa fedha hususani  wao wabunge mapaka sahivi  hakuna hata  mbunge aliyepata hata mshahara.




        Umoja huo wa UKAWA ni muunganiko wa Vyama vya CHADEMA,CUF na NCCR pamoja NLD.

Tags:

Share This Post

Get Updates

Subscribe to our Mailing List. We'll never share your Email address.

0 comments:

Total Pageviews

back to top